21st December, 2020
Benson kang’ara mutura ameapishwa kuwa kaimu gavna wa kaunti ya nairobi katika kipindi cha siku 60 ambapo kwa mujibu wa katiba, iebc inatarajiwa kuandaa uchaguzi mdogo kabla ya siku hizo kukamilika. Anavyoarifu mwanahabari geff kirui , dakika chake baada ya kula kiapo , mutura alitia saini agizo litakalowezesha wizara ya fedha kutoa takriban shilingi bilioni 37.5 ya bajeti ya kaunti ya nairobi ambayo mike sonko alikuwa amekaidi kutia saini kufuatia mvutano kati yake na mkurugenzi wa nms meja mstaafu mohammed badi.