9th December, 2020
Washukiwa 11 kati ya 12 ambao wote ni jamaa wa familia moja wanaohusishwa kwenye mauaji ya marehemu juliana mwikali ngui, wamenyimwa dhamana na mahakama ya machakos. Washukiwa hao 11 wamekuwa wakizuiliwa katika gereza la machakos na wamekuwa wakihudhuria vikao vya mahakama kupitia mtandao wa skype. Mwikali aliuawa nyumbani kwake katika kijiji cha kathuma kaunti ya machakos mnamo agosti mbili mwaka huu. Kulingana na judge david kemei, washukiwa hao hawangepewa dhamana kutokana na usalama wao na jinsi hali ilivyo kwa ssa kijijini mwao.