.
25th November, 2020
Wakazi wa eneo la Kapkatet kaunti ya Kericho, waliachwa vinywa wazi, baada ya jamaa aliyedhaniwa kuwa amefariki, kugutuka akiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti. Inaarifiwa kuwa Peter Kiplangat Kigen aligutuka wakati mhudumu wa chumba cha kuhifadhi maiti alipokuwa akikata sehemu ya mwili yake ili kuweka dawa ya kuhifadhi maiti yake. Alipelekwa chumba cha kuhifadhi maiti baada ya kudhaniwa kuwa amekufa ghafla baada ya kuanguka.