18th November, 2020
Mkurugenzi wa Elimu katika Kaunti ya Uasin Gishu Mbaka Gitonga ambaye alisemekana kudahlilishwa na Waziri wa Elimu Prof George Magoha alipozuru kaunti hiyo wiki mbili zilizopita amehojiwa na Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi EACC. Mbaka ametakiwa kuandikisha taarifa kuelezea kilichojiri na kumsababisha Waziri Magoha kumtukana hadharani. EACC imethibitisha kuwa uchunguzi unaendelea kuhusiana na tukio hilo. Wiki mbili zilizopita waziri magoha alipozuru Shule ya Msingi ya Langas mjini Eldoret alinaswa kwenye video akitumia maneno ya matusi dhidi ya Mbaka Gitonga kisa ambacho kilikashifiwa vikali.