18th November, 2020
Viongozi na wakazi wa eneo la Mtepeni kaunti ya Kilifi wanaitaka tume ya maadili na kupambana na ufisadi EACC kuchunguza kandarasi ya shilingi milioni 56 iliyotolewa kwa ujenzi wa daraja la Mto Mkuu, mto unaoaminika na wenyeji kuwa na mazingaombwe baada ya vifo vya zaidi ya watu kumi ndani ya kipindi cha miaka miwili iliyopita. Ila tangu mwezi Oktoba mwaka jana wakati ujenzi rasmi ulianza hakuna chochote kinachoendelea kwa sasa.