.
18th November, 2020
Watu kumi wanaosemekana kuwa Raia wa Uganda wamethibitishwa kufariki katika mkasa wa boti uliotokea mapema hii leo katika eneo la Usenge kaunti ya Siaya. Taarifa zinasema kuwa boti hiyo ilikuwa ikisafirisha mizigo kutoka nchini Uganda ikiwa na takriban abiria ishirini. Oparesheni ya kuopoa miili ya abiria kumi wanaosemekana kuwa Raia wa Uganda walioangamia kwenye mkasa huo inaendelea ambapo kufikia sasa tunaarifiwa ni mwili mmoja utu ambao umeopolewa kutoka kwa maji.