11th November, 2020
Madai ya ukiukaji wa haki za binadamu na kampuni ya Kakuzi yameathiri sekta ya zao la maparachichi nchini. Washikadau katika sekta hiyo wanasema uchunguzi unaoendelea dhidi ya kakuzi baada ya madai hayo kuibuliwa na kampuni za uingereza, sainsbury na lidl utaathiri sekta kwa muda kabla ya kurejelea hali ya kawaida.