11th November, 2020
Serikali ya kaunti ya Kisumu imetoa ilani kwa wenyeji wanaoishi mitaa inayokaribia makao makuu ya mji huo kutowazika wapendwa wao kwenye maboma yao. Mazishi katika mitaa kama Obunga, Nyalenda, Manyatta, Bandani nna Kondele sasa hayatakubaliwa hasa kwa wale wanaomiliki mashamba wanamoishi. Hatua hii ambayo inafaa kuimarisha hadhi ya Kisumu kuwa mji, inapingwa na wenyeji ambao wataathirika na sheria hii.