.
8th November, 2020
Wazazi wawili leo hii wameunganishwa na wanawe waliokuwa wamepotea tangu mwaka jana. Watoto hawa ambao walikuwa majirani katika mtaa wa mukuru kwa njenga walikuwa katika nyumba ya kuhifadhi watoto ya Emmanuel Rescue Center mtaa wa Kayole Soweto. Kurudiana huku kwa wazazi na watoto wao imefanikishwa na mitandao ya kijamii.