.
2nd November, 2020
Wachezaji wa timu ya taifa ya kandanda Harambee stars pamoja na kikundi cha ukufunzi hii leo walipimwa virusi vya korona kabla kuingia kambini rasmi kwa maandalizi ya kuchuana na timu ya Comoros kwenye mashindano ya kufuzu kombe la bara afrika. Mechi hiyo itaandaliwa tarehe kumi na moja mwezi Novemba kabla mechi ya marudiano siku nne baadaye.