.
30th October, 2020
Waziri wa elimu, Profesa George Magoha, amefutilia mbali Uwezekano wa shule kufungwa tena kwa sababu ya Ongezeko la maambukizi ya COVID-19 akizungumza katika Kaunti ya kisii baada ya kuzuru shule ya sekondari ya Wasichana ya kereri, waziri magoha alisema licha ya idadi ya Maambukizi kupanda, wanafunzi wa gredi ya nne, darasa la Nane na kidato cha nne wataendelea na masomo yao. Aliongeza kwamba ingawa serikali ipo chini ya shinikizo la Kufungua shule zote, uamuzi kuhusu suala hilo utafanywa Baada ya majadiliano na wadau.