.
20th October, 2020
Zaidi ya wasichana 2000 kutoka familia maskini katika kaunti za isiolo, marsabit na samburu watapokea sodo za kutumia kwa mwaka mzima, kama njia moja ya kuhakikisha wanaendelea na maisha yao inavyofaa hata wakati wa hedhi. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo, mwelekezi wa mradi wa maendeleo wa nawiri john leshalote, wasichana wengi kutoka familia maskini wamekuwa wakitegemea kupewa sodo wakiwa shuleni, hali hiyo imewafanya kutaabika sana hasa wakati huu ambao wamesalia nyumbani kwa kipindi kirefu kutokana na korona.