.
14th October, 2020
Zoezi la kuwaajiri walimu katika kaunti ndogo ya Bunyala eneo bunge la Budalangi kaunti ya Busia lilikumbwa na vurumai baada ya wakazi wa eneo hilo kuingilia kati na kuwafurusha baadhi wa walimu waliokuwa wamejitokeza kwa shughuli hiyo kutoka nje ya kaunti ndogo ya Bunyala. Baadhi ya waliofurushwa wamelaani kitendo hicho na kukitaja kuwa dhuluma kwao baada ya kutuma maombi ya kazikwa njia ya mtandao na kupewa idhini ya kuhudhuria shughuliya kaguliwa kwa stakabadhi zao.