.
7th October, 2020
Mahakama ya nairobi imewapata na hatia washukiwa wawili kati ya watatu waliohusishwa na shambulizi la kigaidi la Westgate lililotokea miaka saba iliyopita. Washukiwa hao Mohamed Ahmed Abdi na mwenzake Adan Hussein Mustafa wanadaiwa kushirikiana kutekeleza ugaidi pamoja na kusaidia wakati wa shambulizi hilo. Mshukiwa mmoja liban abdullahi hata hivyo aliachiliwa huru kwa kukosa ushahidi wa kutosha.