1st October, 2020
Kwenye matukio yanayoashiria changamoto za baada ya ukoloni barani afrika, jamii za wanubi nchini kenya na ile ya washona sasa zimerejelea wito wa kutaka kupewa rasmi uraia wa kenya. Jamii hizo zinasema kukosa vitambulisho, vyeti vya kuzaliwa na uraia kunawakandamiza kiuchumi, kisiasa na kuwanyima haki za kimsingi.