1st October, 2020
Wizara ya elimu ikiendelea na mpango wa kuandaa shule kwa minajili ya ufunguzi shule za wanafunzi wanaoishi na ulemavu zimeonekana kutengwa na serkali katika shughuli zake. Baadhi ya shule hizo hazina madawati pamoja na vifaa vingine ambavyo ni muhimu kuzuia msambao wa virusi vya korona huku nyingine zikikosa kabisa ufadhili.