.
25th September, 2020
Wafanyakazi katika hospitali ya kitaifa ya kenyatta   waliandamana mpaka ofisi za tume ya kuratibu mishahara nchini (SRC) kutaka mishahara yao iratibiwe kulingana na mkataba ulioafikiwa mwaka wa elfu mbili kumi na mbili.wafanyakazi hao kutoka muungano wa madaktari nchini KMPDU, muungano wa wauguzi na muungano wa wafanyakazi   wa kudheiha, wameipa tume hiyo makataa ya siku mbili
  kuratibu mishahara la sivyo hawatorejea kazini kuanzia
  jumatatu.