26th August, 2020
Naibu mkuu wa Chuo Kikuu cha Maasai Mara Prof Mary Walingo na washukiwa wengine wanne wameachiliwa kwa dhamana ya shilingi Milioni Ishirini kila mmoja au mdhamini wa shilingi milioni kumi kila mmoja. Watano hao wameshtakiwa kwa makosa ya Uhalifu wa Kiuchumi baada ya kutumia bila maelezo shilingi milioni 177. Wakati huo huo Gavana wa Migori Zachary Okoth Obado pamoja na wanawe wanne wamezuiliwa na Polisi wakisubiri kufikishwa mahakamani hapo kesho kwa Tuhuma za Ufisadi.