.
13th August, 2020
Watu watatu wameteketea hadi kufa huku mtoto wa miaka mitatu akiokolewa akiwa na majeraha mabaya ya moto katika kijiji cha Munyanja eneo bunge la Funyula kaunti ya Busia baada ya nyumba walimokuwa wamelala kuteketezwa usiku wa kuamkia leo. Inadaiwa nyumba hiyo iliwashwa moto na mshukiwa mmoja baada ya kukataliwa na mpenziwe aliyekuwa amemrithi baada ya kifo cha mke wake.