.
13th August, 2020
Kiongozi wa ODM raila odinga amesema sharti kura ya maamuzi ifanywe kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2022. Raila amesema kampeini za kupigia upato mapendekezo kwenye ripoti ya BBI itazinduliwa tena hivi karibuni pindi tu kiwango cha maambukizi ya virusi vya korona kitakapopungua nchini. Mojawapo ya mapendekezo yanayotarajiwa kwa hamu na wanasiasa ni kubuniwa kwa nyadhifa zaidi za uongozi ikiwemo wadhifa wa waziri mkuu mwenye mamlaka, pamoja na kuongeza mgao wa pesa mashinani hadi asilimia thelathini na tano.