17th June, 2020
Ni afueni kwa wafanyabiashara wanaotumia kivuko cha
mpaka wa namanga, baada ya waziri wa jumuiya ya afrika
mashariki aden mohammed kuufungua mpaka wa namanga na
kuwaruhusu wafanyibiashara wa mataifa hayo kuendelea na
biashara zao
ni majuma mawili hivi tangu mpaka huo kufungwa katika
kudhibiti maambukizi ya virusi vya korona na waziri
mohammed wameafikiana na upande wa tanzania kuufungua
mpaka huo huku madereva wakipimwa kabla ya kuingia au
kutoka upande mwengine. Awali, madereva wa masafa
marefu kutoka nchi jirani ya tanzania na ambao hapo mbeleni
walikuwa wanakataa kupimiwa humu nchini, sasa wamekubali
kuwa wakipimiwa humu nchini bila tashwishi yoyote