.
12th June, 2020
Kamati ya nidhamu ya chama cha kanu imemuonya gavana wa
pokot magharibi prof john lonyangapuo dhidi ya kuvuruga
sera za chama. Kamati hiyo inayosimamiwa na aliyekuwa
seneta maalum zipporah kittony imesema ni makosa kwa
gavana huyo kuchochea waakilishi wadi 15 wa chama hicho
wanaokabiliwa na shutma za kinidhamu kupuuza kufika mbele
ya kamati hiyo. Inadaiwa lonyangapuo aliwashauri waakilishi
hao, 12 kutoka pokot magharibi na 3 kutoka baringo
kutoheshimu wito wa kufika mbele ya kamati hiyo baada ya
kuripotiwa kwenda kinyume cha katiba ya chama.