20th May, 2020
Rais john magufuli wa tanzania amewataka viongozi wa
mikoa iliyopo mipakani mwa tanzania pamoja na waziri wa
uchukuzi nchini humo wakutane na viongozi wa kenya ili
wazungumze kwa lengo la kuleta muafaka katika malumbano
yaliyojitokeza kuhusu udhibiti wa homa ya korona. Rais
magufuli ameyasema hayo aliposimama mkoani singida
akitokea chato kuelekea dodoma ambapo amesema, rais
uhuru kenyatta alipompigia simu na kuzungumzia suluhu
ya homa ya korona, isisababishe mikwaruzo kwani ipo siku
itapita na maisha lazima yaendelee.