.
18th December, 2019
Kiongozi wa chama cha ANC Musalia Mudavadi amezindua kitabu cha wasifu wake, kinachoangazia maisha yake kutoka utotoni, alipoingia siasani hadi kufikia sasa. Mudavadi alizindua kitabu hicho kwenye hafla iliyohudhuriwa na vinara wenza katika muungano wa nasa Moses Wetangula na Kalonzo Musyoka, pamoja na waziri wa michezo Amina Mohammed. Mudavadi anawataka wanasiasa wenza pia kuandika vitabu vyao kama mojawepo ya mbinu za kuhifadhi historia ya nchi.