.
1st April, 2019
Gavana wa Kajiado Joseph ole Lenku amemshambulia Mbunge wa Kajiado Mashariki Peris Tobiko, kwa madai kwamba mbunge huyo anaonyesha madharau ndani ya chama cha jubilee. Lenku alizungumza hayo katika kanisa la anglikana la st. Peter's huko kajiado, wakati naibu rais william ruto alifika kanisani humo kusaidia mchango wa fedha za kanisa hilo. Peris tobiko amekuwa mkosoaji sugu wa gavana lenku na inaarifiwa anajiandaa kuwania kiti cha ugavana kwenye uchaguzi mkuu ujao.