25th March, 2019
Waziri wa usalama wa ndani, daktari fred matiang’i, amezitaka wizara na idara zote za serikali kukoma mara moja ununuzi wa sare na mavazi rasmi kutoka nje. Matiang’i, ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati kuu ya serikali kuhusu ustawi na utekelezaji wa miradi, amesema uagizaji wa bidhaa muhimu kama vile mavazi kutoka mataifa ya nje ni kudhoofisha uchumi wa nchi. Matiang'i aliyasema hayo alipoyatembelea makao makuu ya nys kukagua ushonaji wa sare za polisi.