12th March, 2019
Mataifa zaidi yamepiga marufuku usafiri wa abiria kwa ndege aina ya 737?800 max kama njia ya tahadhari baada ya ndege mbili za aina hiyo kuhusika kwenye ajali katika kipindi cha miezi mitano. Mataifa mengine yameharamisha usafirishaji wa abiria kwa ndege aina hiyo kupitia anga zake. Mataifa hayo ni kama vile uingereza, singapore, indonesia, uchina na ethiopia. Wakati huo harakati za kusafirisha familia za waliofariki kwenye mkasa wa ndege wa ET302 kuelekea nchini ethiopia kutambua miili ya wapendwa wao zinaendelea. Familia zinalalamika kuhusu kucheleweshwa kwa utoaji wa taarifa muhimu kuhusu mkasa huo.