.
11th February, 2019
Utata umeibuka kuhusu ujenzi wa madarasa mawili katika chuo anuwai cha Kabula katika Kaunti ya Bungoma. Wakazi na bodi ya usimamizi wa chuo hicho wameusimamisha ujenzi wa mradi huo uliotengewa kima cha shilingi milioni mbili nukta nne ili uchunguzi ufanywe kubaini ni vipi ujenzi wa madarasa mawili uligeuzwa na kuwa darasa moja na choo kimoja cha shimo.