.
19th January, 2019
Mtu aliyezingatiwa kuwa na nguvu zaidi Barani Afrika na wa pili kwa nguvu kote duniani Conrad Njeru Karukenya almaarufu Tiger Power amezikwa hivi leo nyumbani kwake katika kijiji cha makengi eneo Bunge la Runyenjes kaunti ya Embu. Hali ya majonzi kutoka kwa familia ya Tiger Power ilitanda katika hafla ya mazisha hayo ambayo ilihudhuriwa na gavana wa kaunti ya embu martin wambora na viongozi wengine.