.
4th January, 2019
Wazazi walivamia shule ya msingi ya Lalagin eneo la Bureti na kisha kumtimua mwalimu mkuu. Kundi hilo la wazazi waliojawa na hasira limedai kuwa mwalimu mkuu ndiye wa kulaumiwa kutokana na matokeo duni ya wanafunzi wa shule hiyo katika mtihani wa kitaifa. Mwalimu huyo mkuu hakuweza kupatikana mara moja kujibu shutuma hizo.