8th December, 2018
Mahangaiko yaliyoshuhudiwa miongoni mwa wasafiri jijini Nairobi siku ya jumatatu ya wiki hii yaliweka bayana udhaifu uliopo kuhusiana na mfumo wa uchukuzi wa umma humu nchini. Huku Kenya ikijaribu kuweka mikakati kuimarisha mfumo wa uchukuzi, nchi ya Ufaransa imepiga hatua kubwa katika sekta hii na kwa hivi sasa, hawana changamoto kama zinazoshuhudiwa humu nchini bali mwelekeo wao sasa ni kuangazia mbinu za uchukuzi zinazosaidia kuhifadhi mazingira. Mhariri wetu daniel korir amekuwa jijini paris ufaransa na kutuandalia taarifa ya namna taifa hilo sasa linafanya jaribio la kutengeneza magari ya kutumia umeme ambayo amini usiamini hayatahitaji madereva.