.
28th November, 2018
Katika kisa cha kusikitisha…Dennis Kimani, mwanamme mwenye umri wa makamo aliuwawa kinyama. Dennis ambaye alikuwa kiziwi alikumbana na mauti yake baada ya matatu alimokuwa akisafiria kuelekea katika mtaa wa Kahawa West hapa jijini Nairobi kutekwa nyara na majambazi. Lakini cha kusikitisha zaidi ni kuwa kosa alilofanya Dennis ni kuwa kiziwi. Huku jamaa na marafiki zake wakimpumzisha katika eneobunge la Mathira kaunti ya Nyeri hapo jana, maswali mengi yameibuka kuhusu usalama wa jamaa walio na ulemavu wa kuzungumza na kusikia.