.
26th November, 2018
Afisa mkuu mtendaji wa shirika la bima ya kitaifa ya afya Geoffrey Mwangi na aliyekuwa mkuu wa fedha Wilbur Kurgat watasalia mikononi mwa polisi hadi hapo kesho wakati uamuzi utakapofanyika kuhusiana na mashtaka ya ufisadi yanayowakabili. Mawakili wao wakiongozwa na profesa tom ojienda wamefaulu kuhakikisha kuwa hawali kiapo wakidai kuwa mashtaka dhidi yao yalijengwa nje ya sheria. Mwanahabari francis ontomwa amefuatilia kesi hii mahakamani na sasa anaelezea ni kwani nini kesi hii inatarajiwa kugusa nyoyo za wakenya.