16th October, 2018
Na leo ni siku ya chakula duniani; kauli mbiu ya maadhimisho ya siku hiyo mwaka huu ni 'matendo yetu, ni mustakabal wetu'. Katika maadhimisho ya siku ya chakula duniani, shirika la umoja wa mataifa kuhusu kilimo na chakula?fao linalenga kuhakikisha kuwa dunia haishuhudii tena baa la njaa ifikapo mwaka 2030. Hapa nchini maadhimisho ya siku hii yalifanyika katika eneo la njoro kaunti ya nakuru na kuhudhuriwa na maafisa kutoka wizara ya kilimo.