.
15th October, 2018
Maskwota katika eneo la Sabaki eneo bunge la magharini Kaunti ya Kilifi walizua kizaazaa pale walipovamia iliyokuwa ardhi ya shirika la ustawi wa kilimo nchini adc na kufanya tambiko ili kuwalaani watu ambao wamedai kuwa ni wanyakuzi wa ardhi hiyo ambayo ilirejeshwa kwa jamii. Wakaazi hao hatimaye walianza kujigawia ardhi hiyo wakisisitiza kuwa ni wao ndio wamiliki halali.