.
15th October, 2018
Zaidi ya wakazi alfu 25 wanaoishi katika kijiji cha Lesesia eneo Bunge la Taveta kaunti ya Taita Taveta wanaishi kwa wasiwasi baada ya kupokea amri na vitisho vya kutimuliwa katika kijiji hicho kutokana na utata wa umiliki wa timbo za mawe zilizoko katika kijiji hicho. Kulingana na wakazi hao viongozi kutoka eneo hilo ndio wanaowahangaisha wakitaka kuchukuuwa usimamizi wa shughuli zote za uchimbaji mawe ambazo zimekuwa zikiwapa mkate wao wa kila siku kwa miaka na mikaka.