.
2nd October, 2018
Mwanahabari wa Standard James Omoro anauguza majeraha baada yaafisa mmoja wa polisi kumgeukia na kumpiga na hivyo kumjeruhi vibaya wakati akifanya kazi yake katika majengo ya bunge la kaunti yamigori. Omoro alikuwa anafuatilia vuta nikuvute ambayo imegubika bungehilo, swala kuu likiwa utata unaozingira nafasi ya kiongozi wa wengi bungeni. Rabsha zilizuka katika bunge hilo na wakati omoro alipojaribu kupigapicha, afisa mmoja wa polisi alimgeukia na kumpiga vibaya na kuiharibu kamera yake.