26th September, 2018
Gavana wa kaunti ya Busia Sospeter Ojaamong amewahakikishia wakaazi wa kaunti hiyo kuwa miradi ya maendeleo ambayo ilikuwa imekwama sasa itaanza kutekelezwa baada ya kaunti hiyo kupokea pesa kutoka kwa serikali kuu. Ojaamong ambaye anakabiliwa na mashtaka ya ufisadi alikuwa akizungumza katika kijiji cha mayenje,eneo bunge la Matayos wakati akikagua mradi wa ujenzi wa barabara inayofadhiliwa na serikali ya kaunti.