.
24th September, 2018
Washukiwa kumi wa kundi la wanamgambo wa alshabaab wameripotiwa kuuwawa na wanajeshi wa Kenya katika eneo la Pandanguo Kaunti ya Lamu . Kadhalika wanajeshi wa kenya wamenasa bunduki saba aina ya ak 47 kutoka kwa wanamgambo hao. Taarifa zinasema kuwa wanajeshi watatu wamejeruhiwa katika makabiliano hayo. Wakaazi wa lamu wameelezea kuridhishwa na juhudi zinazoendelea za kupambana na wanamgambo hao.