.
20th September, 2018
Makachero wa tume ya maadili na kupambana na ufisadi, EACC, wamezitwaa stakabadhi muhimu zake aliyekuwa Gavana wa Nairobi, Dr Evans Kidero na watoto wake wawili.
Kidero ameyathibitisha hayo kwa kuelezea mshangao wake kwani miongoni mwa pasi za usafiri zilizotwaliwa ni ya marehemu mwanawe aliyefariki miaka kadhaa iliyopita. Hata hivyo Kidero kupitia wakili wake, Peter Wanyama, ameapa kupinga hatua hiyo mahakamani kwa misingi kwamba utaratibu wote ulikiuka haki zake za msingi.