.
3rd September, 2018
Waziri wa Usalama Dr. Fred Matiang'i amesema wizara yake inabuni mpango wa kutoa suluhu la kudumu la kutoa usalama wa kutosha katika ziwa victoria ili kukabiliana na malalamiko mengi ambayo hutolewa mara kwa mara na wavuvi wa humu nchini. Akizungumza katika kaunti ya nyanza wakati wa mkutano wa usalama, dkt matiang'i amesema kuna kitengo kinachoshughulikia mpango huo ambao utashughulikia kikamilifu swala la usalama katika victoria.