30th July, 2018
Mwili wa msichana wa umri wa miaka kumi na mitatu ulipatikana katika shamba la mahindi sehemu ya kwa Tom, katika kaunti ya nakuru, ikiarifiwa kwamba alibakwa na kisha kuuawa. Kulingana na majirani, esther muthoni aliyekuwa mwanafunzi wa shule ya msingi ya engashura, alitumwa dukani na mamake jana jioni, lakini hakurejea. wakazi wa mtaa huo wamewasuta polisi kwa utepetevu kutokana na ongezek la visa vya utovu wa nidhamu. Wanataka uchunguzi wa haraka kufanywa ili kubaini aliyetenda unyama huo.