.
15th February, 2018
Bingwa wa dunia katika mbio za mita 5000 Hellen Onsando Obiri amepewa tiketi ya moja kwa moja kushiriki mashindano ya jumuiya ya madola bila ya kupitia njia ya mchujo. Obiri ni miongoni mwa wanariadha mahiri waliotuma ombi kwa shirikisho la riadha nchini kutoshirikishwa katika mchujo utakaoandaliwa wikendi hii uwanjani Kasarani.