.
6th December, 2016
Wabunge saba waasi katika chama cha ODM, gavana, na naibu gavana huenda sasa wana hesabu siku saba tu kisha wapoteze nyadhifa zao na kusukumwa kwenye uchaguzi mdogo wakati wowote kuanzia sasa. Baada ya kupokea maamuzi ya mwisho kutoka baraza kuu la uongozi la ODM, msajili wa vyama vya kisiasa Lucy Ndung’u sasa amewaandikia barua viongozi walioadhirika kuwafahamisha kwamba atawaondoa kwenye sajili ya wanchama wa ODM katika muda wa siku saba zijazo, na hivyo basi wapoteze viti vyao vya uongozi.