.
27th November, 2016
Hali ya wasiwasi inazidi kughubika maeneo ya mpakani kaunti za Baringo na Turkana baada ya mashambulizi yanayohusishwa na wizi wa mifugo. Kufikia sasa takriban ng’ombe 1900 pamoja na mbuzi 700 wameibwa huku watu 14 wakiuawawa wengine wakiuguza majeraha ya risasi.