26th November, 2016
Maabara kubwa ya uchunguzi wa vimelea vya ugonjwa wa kifua kikuu (TB) kwa kutumia panya imezinduliwa mjini Dar Es Salaam nchini Tanzania ikiwa ni mkakati wa kupambana na ugonjwa wa kifua kikuu unaowapata watanzania laki moja na sitini kwa mwaka. Hii ni kwa mujibu wa takwimu za Wizara ya Afya nchini humo.