.
23rd November, 2016
Katibu mkuu wa COTU Francis Atwoli hii leo amepokea ripoti ya utafiti uliofanywa kuangazia kiongozi yupi wa jamii ya Waluhya aliye na umaarufu sana ambaye atawania urais katika uchaguzi mkuu ujao. Atwoli alichukua jukumu hilo katika azma yake ya kuhakikisha kuwa jamii ya Waluhya imeungana kumtafuta kiongozi mmoja atakayemenyana na viongozi wengine katika uchaguzi mkuu wa mwaka kesho. Utafiti huo uliongozwa na Dr. Fred Jonyo wa chuo kikuu cha Nairobi.