.
17th November, 2016
Idadi kubwa ya Wakenya inahofia zaidi wapiganaji wa Al Shabab wenye mako yao Somalia. Katika utafiti uliofanywa na shirika la Twaweza East Africa kati ya Wakenya kumi, tisa wana hofu kubwa na matukio yanayotekelezwa na kundi la Al Shabab. Vivyo hivyo idadi kubwa ya Wakenya inataka kambi ya wakimbizi ya Dadaab kuondolewa kabisa halikadhalika wanajeshi wa Kenya walio Somali kurejeshwa nyumbani.