5th November, 2016
Askofu mkuu wa kanisa katoliki dayosisi ya Embu Paul Kariuki amepiga marufuku wanasiasa kufanya harambee kanisani katika eneo hilo hadi kukamilika kwa uchaguzi mkuu ujao . Kariuki amewaandikia barua mapadre wote katika Dayosisi yake na kuwataka wasiwakaribishe wanasiasa kuwa wageni wa harambee zao. Kariuki amewataka wanasiasa kuendesha shughuli zao za kisiasa katika mikutano ya siasa na wala sio makanisani . Askofu huyo pia ametoa onyo dhidi ya viongozi kanisani watakaochukua misimamo ya kisiasa. Anasema kuwa wanasiasa wanatumia kanisa vibaya kutafuta kura .