.
2nd November, 2016
Chama cha Wiper kimeteua kamati maalum ya watu kumi kuchunguza waasi wa chama ambao ni wabunge wanne pamoja na gavana mmoja walioondoka chamani humo. Wanaonuiwa kuchunguzwa ni pamoja na gavana Alfred Mutua, wabunge John Munuve, Joe Mutambu, Katemi Makenga na Regina Ndambuki. Aidha kamati ya kuwachunguza tano hao itaongozwa na Haron Ndubi.